
Muda mfupi baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, kuagiza Jeshi la Polisi kumuachia huru Msanii Nay wa Mitego ambaye alikuwa akishikiliwa na Jeshi hilo kwa tuhuma za wimbo wake wa ‘WAPO’ kutokuwa na maadili, Nay wa Mitego ametoka kituoni hapo leo March 27 2017.
