TAARIFA KUTOKA BRAZIL,KEPTEN MPYA ATAJWA - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Thursday, 23 March 2017

TAARIFA KUTOKA BRAZIL,KEPTEN MPYA ATAJWA

BEKI wa Inter Milan Miranda ndie amepewa Utepe wa Kepteni wa Brazil wakati Ijumaa Alfajiri ikicheza Ugenini huko Mjini Montevideo na Uruguay katika Mechi ya Kundi lao la Nchi za Marekani ya Kusini ya kusaka Washiriki wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia.

Baada ya Kepteni wa Brazil Neymar kujiuzulu wadhifa huo Julai Mwaka Jana na tangu ashike madaraka Juni 2016 Kocha wa Brazil Tite alisema atakuwa hana Nahodha wa kudumu na badala yake kuuzungusha Utepe wa Kepteni miongoni mwa Wachezaji vingunge wa Kikosi chake.

Miranda ndie alikuwa Kepteni wa kwanza wa Kikosi cha kwanza kabisa cha Tite Brazil ilipoichapa Ecuador 3-0 huko Quito Septemba 2016.

Wengine waliowahi kuuvaa Utepe huo ni Dani Alves mara 2 (dhidi ya Colombia na  Argentina), Fernandinho (Peru), Filipe Luis (Venezuela) na Renato Augusto (Bolivia) zote zikiwa Mechi za Kundi lao za Kombe la Dunia 2018.


Pia, Robinho na Diego walikuwa ndio Manahodha Brazil ilipocheza Kirafiki na Colombia Mwezi Januari kwenye Mechi ambayo Kikosi cha Tite kiliundwa na Wachezaji waliokuwa wakicheza ndani Nchini Brazil pekee.