Kwa tafasiri ya haraka inaweza kuwashangaza watu wengi na kuhoji
nini kulikoni kwa mtumishi wa umma tena mwenye taaluma ya kufundisha
kwa ngazi ya elimu ya sekondari, kufikia hatua ya kuacha taaluma hiyo na
kuingia kwenye ajira binafsi ya ushereheshaji wa hadhira(MC). Lakini moja kati ya changamoto kubwa zinazoikabili
Serikali katika sekta ya elimu ni kilio cha walimu kupata mishahara
kidogo, kukosa makazi ya kuishi na vitendea kazi, mchango kidogo kwa
Serikali na mtazamo hasi uliopo katika jamii.
Mambo hayo yanaweza kuwa sababu ya mwalimu
Emmanuel Mathias (28), kutoka shule ya sekondari ya DCT Jubilee iliyopo
mkoani Dodoma, ambaye ameacha ualimu na kuwa kati ya ma- MC maarufu hapa
nchini. Hakupata wakati mgumu na haoni sababu ya kujutia
kabisa uamuzi huo baada ya kuacha taaluma hiyo kwa kipindi cha miaka
miwili iliyopita. Alifahamika kwa jina la mwalimu Emmanuel lakini kwa
sasa ni MC Pilipili......READ MORE
