Alifahamika kwa jina la mwalimu Emmanuel lakini kwa sasa ni MC Pilipili.
Manjonjo, vituko na uwezo mkubwa wa ‘kuchekesha’ jukwaa ndiyo umechangia kubadilisha taswira yake aliyonayo kwa sasa..
Pilipili anasema ameanza kuifanya kazi hiyo tangu mwaka 2003, akiwa ni mwanafunzi wa shule ya sekondari. “Kwa kipindi cha miaka kumi sasa nimefanikiwa kujenga nyumba, ninasomesha wadogo zangu watatu katika ngazi za Chuo Kikuu na sekondari,” anasema.

