Msanii wa bongo movies Flora mvungi ambaye hivi majuzi alifunga
ndoa ya kimya kimya na msanii mwingine kwenye upande wa bongo fleva
amewataka watu wote walioanza kuichokonoa ndoa yake hiyo kwa kauli kuwa “itadumu mwaka mmoja tuu” wamuache
kwa amani kwani itadumu milele kwakuwa yeye na H-baba wanapendana na
wamekuwa wakichunguzana tabia kwa muda mrefu kabla ya kuamua kuoana.
Katika mahojiano aliyoyafanya na mwandishi wa mtandao wa global
publishers Imelda Mtema, flora mvungi amesema yeye na mpenzi wake huyo
walishakaa muda mrefu na kuchunguzana, hawakukurupuka kuingia kwenye
ndoa hivyo siyo rahisi kuachana kwa midomo ya washakunaku kama
walivyotabiri.
“Wanikome! Wanaongea tena… alimalizia Flora mvungi.
