
Chini ya mwezi
mmoja baada ya kumsajili Mbrazil Tiago
Franc Lino Alves na Mburundi Fuadi Ndayisenga, SC Villa "Jogoo" imesaini nyota mwingine
mgeni, Boue Bi Marc Olivier aliyekuwa anacheza klabu ya Atlantis FC inayoshiriki Ligi daraja la Tatu.
Mshambuliaji
huyo wa Ivory Coast amesaini mkataba wa
miaka miwili na Villa ambapo Raisi wa
klabu hiyo Ben Immanuel Misagga
alimtangaza mbele ya wanahabari mchezaji huyo.
"Nina
furaha bado kutangaza mshambuliaji mwingine mpya kutoka Ivory Coast, Lengo letu ni kushinda Ligi Kuu msimu huu na
tunaweza tu kushinda kwa kufunga mabao. Sisi tumemkubali ni mtu bora kwetu alikuwa anacheza Atlantis
kutoka Kwao ambapo yeye anadai kuwa
amefunga mabao 10 msimu uliopita kwahiyo ni mchezaji mzuri sana.
Boue Bi
anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza kesho Jumanne nyumbani kwa Soana Fc ambao wamefungwa mabao matatu tu baada ya
mechi sita.