
Chris Smalling amemsapoti Wayne Rooney na kutamka huyo ndie 'Mtu Mkuu' kwa Manchester United na England.
Kauli hii imekuja baada ya Jumamosi Rooney kupigwa Benchi na Meneja
Jose Mourinho kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, dhidi ya Mabingwa
wa England Leicester City ambayo Man United walishinda 4-1 huku Bao zao
zote zikifungwa Kipindi cha Kwanza.
Kuhusu kumtema Rooney, Mourinho alitoboa uchezaji wake umeathiriwa
na kupondwa mno wakati akiichezea England ambayo yeye pia ndie Kepteni
kama alivyo kwa Man United.
Mara baada ya Mechi hiyo na Leicester, Mourinho alipasua kuwa Wayne Rooney bado ni Mchezaji mkubwa kwa Timu yao.
Mourinho alisema ana imani yote kwa Rooney na kuwa bado ni Mchezaji muhimu kwa Timu yao licha ya kumuanzisha Benchi.
Hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Rooney kutoanza Mechi chini ya
Mourinho na mara ya mwisho kwa Kepteni huyo kupigwa Benchi ni Desemba 26
Mwaka Jana.
Mourinho alieleza: "Ni Mtu wangu, namuamini kwa kila kitu. Yeye ana furaha kama mimi na hii ndiyo Timu."
Aliongeza: "Yeye ni Mchezaji mkubwa kwangu mimi, United na ni Mchezaji mkubwa kwa Nchi hii!"