TANZIA: BABA MZAZI WA BELLE 9 AFARIKI DUNIA - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Tuesday, 18 April 2017

TANZIA: BABA MZAZI WA BELLE 9 AFARIKI DUNIA

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Abelnego Damian “Belle 9” kwa taarifa zilizotufikia katika chumba chetu cha habari kuwa baba yake mzazi mzee ‘Damian Nyamonga’ amefariki dunia kwa ajali ya boda boda .
Akizungumza na Capitaltz.com meneja wa Belle 9 Jahz Zamba amethibitisha taarifa hiyo kwa kusema “ni kweli baba yake Belle 9 amefariki nataraatibu ni mazishi kesho saa nane kwasababu ameumia sana kwahiyo msiba hauwezi kukaa muda mrefuAlisema.     

"Amegongwa na Boda boda yaani boda boda ilikuwa inatoka speed ikaja ikamgonga kwahiyo hata huyu dereva boda boda ameumia vibaya sana kabla ya kumpeleka hospitali ambako mauti yalimkuta…timu nzima ya vitamini music wameondoka na Belle 9 kwahiyo wapo kwenye kushughulikia masuala yote ili kuwa bega kwa bega na mwenzetu Alisema Jaz.

Kwa niaba ya timu nzima ya Capitaltz.com tunatuma salamu za pole kwa ndugu jamaa na marafaiki walioguswa na msiba huo.