SIMBA NA AZAM HAPATOSHI KESHO TAIFA, NI NUSU FAINALI ASFC - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Friday, 28 April 2017

SIMBA NA AZAM HAPATOSHI KESHO TAIFA, NI NUSU FAINALI ASFC

Vinara wa ligi kuu ya soka Tanzania bara Wekundu wa Msimbazi Simba wametamba kupambana hadi dakika ya mwisho mbele ya Azam FC katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la shirikisho utakaochezwa kesho kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Mratibu wa Simba, Abbas Ally amezungumza na The Capitaltz.com kuhusu maandalizi na matarajio ya kikosi chao ambacho kiliweka kambi ya siku tano mjini Morogoro kwa ajili ya kujiwiwnda na mchezo huo.

Abbas amesema wamejiandaa vyema kuwakabili Azam FC na wana matarajio makubwa ya kupambana vilivyo ili kuhitimisha lengo la kuibuka na ushindi, ambao pia utakua ni sehemu ya kulipiza kisasi cha kufungwa na wana Lambalamba hao katika mchezo wa ligi pamoja na kombe la Mapinduzi mapema mwaka huu.

Kwa upande wa Azam FC, mapema hii leo afisa habari wa mabingwa hao wa Afrika mashariki na kati Jaffary Iddy Maganga  alizungumza na waandishi wa habari kwa ajili ya kuelezea maandaliazi ya kikosi chao ambacho kimedhamria kutoipoteza nafasi ya kuiwakilisha nchi kwenye michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika mwaka 2018.

Jaffary Iddy amesema kikosi chao kipo katika hali nzuri baada ya kufanya maandalizi ya kutosha kwa kipindi cha siku kadhaa, sambamba na kucheza mchezo wa kirafdiki dhidi ya African Lyon juma lililopita.



Hata hivyo Jaffary Iddy amesema pamoja na kuwa na mwenendo mzuri dhidi ya Simba tangu mwanzoni mwa mwaka huu 2017, bado kesho watakwenda uwanja wa taifa wakiwa na tahadhari kubwa kwa kufahamu, mnyama atakua amejiuliza kwa nini alipoteza mara mbili dhidi yao.