Timu ya soka Yanga imeondoshwa katika michuano ya klabu bingwa afrika na timu ya Zanaco baada ya leo hii kutoa suluhu ya 0-0.
Zanaco imefuzu hatua ya pili kwa bao la ugenini baada ya hapo awali kuilazimisha sare ya 1-1 kwenye mchezo uliofanyika uwanja wa taifa jijini Dar Es Salaam.
Yanga leo hii licha ya kuwakosa baadhi ya wachezaji muhimu katika kikosi cha kwanza ,bado walionyesha kuisumbua ngome ya Zanaco lakini bahati haikuwa upande wao.
