AUDIO-ITC YA NGASSA YAWASILI, ATAJWA KUANZA NA MBAO FC - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Thursday, 29 December 2016

AUDIO-ITC YA NGASSA YAWASILI, ATAJWA KUANZA NA MBAO FC

Baada ya kususua kwa takribani majuma mawili sasa  hatimaye  hati ya uhamisho ya kiungo Mrisho Khalfan Ngassa imetua  kwenye klabu ya Mbeya City fc  asubuhi ya leo .
Akizungumza na tovuti ya klabu hiyo muda mfupi uliopita Mwenyekiti wa City, Mussa Mapunda amethibitisha kutua kwa ITC hiyo kutoka shirikisho la soka la Oman ikiwa ni siku chache baada ya klabu ya Fanja  kumruhusu Mrisho Khalfan Ngassa kujiunga na kikosi cha City, ambayo pia  inajulikana  kama  timu ya kizazi kipya.
Akiendelea  zaidi, Mapunda alisema kuchelewa kufika kwa ITC hii hakukuwa na msuguano wowote baina ya vilabu hivi viwili kilichokuwa kinatokea  ni tofauti ya wakati na siku za ufanyaji kazi  kwenye ofisi kulingana  na taratibu za nchi hizi mbili.


Katika hatua nyingine Mapunda amesema kuwa maandalizi kuelekea mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara   dhidi ya Mbao fc uliopangwa kuchezwa jumamosi kwenye uwanja wa Sokoine jijini hapa  yanaenda vizuri  huku imani kubwa kwa uongozi  wa City ikiwa ni kushinda mchezo huo hasa baada ya suluhu katika michezo miwili iliyopita.