Na Baraka Mpenja
BAHATI
haikuwa kwa Yanga usiku huu. Wametolewa na Al Ahly kwa mikwaju ya
penati katika mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika kuwania
hatua ya 16 bora baada ya kufungwa bao 1-0 ndani ya dakika 90.
Mabingwa watetezi, National Al Ahly wamepata penati 4 huku Young Africans wakipata penati 3.
Waliofunga
penati za Yanga ni Didier Kavumbagu `Kavu`, nahodaha na beki wa kati,
Nadir Haroub `Canavaro`, na Emmanuel Anord Okwi .
Wanandinga wa Yanga waliokosa penati usiku huu ni Oscar Samwel Joshua , Said Bahanuzi na Mbuyu Twite .
Mlinda
mlango namba moja wa Yanga Deogratius Munishi ‘Dida’ alipangua penalti
mbili mfululizo ya nne na ya tano, lakini Yanga SC nao wakakosa penalti
mbili mfululizo ya nne na ya tano.
Mbali na kupangua penati hizo, alicheza vizuri ndani ya dakika 90 na kuwa kikwazo kikubwa kwa Al Ahly kupata ushindi.
Mchezo
wa leo umemalizika kwa Yanga kufungwa bao moja sawa na matokeo
waliyoyapata Yanga katika mechi ya kwanza jijini Dar es salaam, Machi
mosi mwaka huu uwanja wa Taifa.
Kusoma zaidi bofya hapa chini