Pia nimejikuta nikiiga sauti yake mara kadhaa na kujirekodi hii ni kutokana na kupenda aina ya utangazaji wake, baada ya kumaliza shule Jamhuri high school Dodoma nilitamani sana kusomea fani hii ambayo ndugu yangu huyu leo amekuwa kinara na mchapakazi mzuri kwenye tasnia ya habari. kwa bahati mbaya nilishindwa na kujikuta nikisomea Tekinohama (IT/ICT) ila ndoto yangu bado inajengwa na kuimarishwa na watu kama Salim Kikeke kwani ameeleza alikotoka mpaka kufanya kitu anachokipenda leo ni Mwandishi na Mtangazaji wa Kipindi bora cha Dakika 30, DIRA YA DUNIA TV (BBC swahili)
Na Msofe James (Blogger - www.thecapitaltz.com)
Tafadhali FUATILIA Mahojiano yake aliofanya na kipindi cha The Avenue - TBC ONE TV

