UHAMIAJI WAZIDISHA MASHARTI YA KUTOA ‘PASIPOTI’ KWA VIJANA - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Friday, 28 June 2013

UHAMIAJI WAZIDISHA MASHARTI YA KUTOA ‘PASIPOTI’ KWA VIJANA

Dar es Salaam. Idara ya Uhamiaji imesema kwa sasa inapata katika kipindi kigumu katika kutoa hati za kusafiria na kwamba imeamua kuwanyima kabisa baadhi ya watu na hasa vijana wanaotaka kwenda nje ya nchi. Imesema hatua hiyo inatokana na vijana wengi kujihusisha na shughuli zisizokuwa halali, zikiwamo biashara ya dawa za kulevya wanapofika katika nchi za kigeni. Hayo yalisemwa jana na Kaimu Msemaji Mkuu wa Idara hiyo, Tatu Burhani, ambaye alisema matukio ya watu kukamatwa na kutumikia vifungo kwa sababu ya kujihuisisha na shughuli hizo, yameifanya idara kuwa makini zaidi katika utoaji wa hati za kusafiria.
“Kwa sasa tutakuwa makini sana katika utoaji wa pasipoti hasa kwa vijana kwa kuwa tumegundua kuwa vijana wengi wakienda nje ya nchi hawana shughuli za kufanya na badala yake, wanaanza kufanya kazi zilizo kinyume na sheria za nchi husika,”alisema Burhani.Alisema idara kwa sasa imeanza kuwawekea masharti vijana ikiwa ni pamoja na ..... SOMA ZAIDI