MSHTAKIWA WA EPA ASIMULIA JINSI WAJANJA WALIVYOMZIDI ‘KETE’ KWENYE AKAUNTI YAKE - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Monday, 24 June 2013

MSHTAKIWA WA EPA ASIMULIA JINSI WAJANJA WALIVYOMZIDI ‘KETE’ KWENYE AKAUNTI YAKE

Godfrey Mosha pichani. Picha na Maktaba 
Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Kampuni ya Principal Ltd, Godfrey Mosha amesimulia jinsi Benki ya Akiba Commercial (DCB), tawi la Kariakoo, ilivyoidhinisha malipo ya fedha kwa mtu mwingine kutoka akaunti yake ndani bila yeye kujua.
 
Mosha ni mmoja wa washtakiwa katika kesi ya  wizi wa fedha kwenye  Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Pamoja na wenzake, Bahati  Mahenge, Manase Makale, Davis Kamungu na Eda Makale, wanakabiliwa na kesi ya wizi wa Sh1.86 bilioni za EPA, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuipitia Kampuni ya Changanyikeni Residential Complex.
Katika kesi hiyo dhidi ya DCB, inayosikilizwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Warialwande Lema, Mosha anaidai benki hiyo Sh46.8 milioni, zilizolipwa kwa mtu asiyemfahamu kwa kutumia hundi nne tofauti na tarehe tofautitofauti....SOMA ZAIDI