MILLARD AYO: Amina.
Tulikuwa
tunasafiri na basi katika safari za kishule, tulikuwa 60 hivi kwenye
basi tukapata ajali ‘Ngongoro crater’ bonde la ufa sehemu inaitwa
‘Malanjo Cross’ ni sehemu hatari sana, yaani tuliingia bondeni, yaani
sidhani kama leo ningekuwa hai.
MO BLOG: Hebu Millard tufafanulie zaidi tukio hilo la ajali lilikuaje..?
MILLARD AYO: Yaani
sina la kusema ila kama Mungu asingependa mimi nisingekuwepo duniani,
lakini kwa sababu alipenda, ndio maana nipo, hata hili kovu katika
kichwa upande wa kushoto lipo. Hapa iliingia chuma, unajua mabasi ya
zamani yalikuwa na chuma, sasa ile chuma ilikatika wakati basi
likijipiga kwenye mawe kama unavyojua kule ni crater.Kwa
kweli ninachokumbuka ni kuwa gari lilipotulia watu walikuwa wakilia na
damu zinatiririka na mimi nilikuwa nimebanwa katika hiyo chuma na
nilipotolewa sikukumbuka tena nini kiliendelea. Ilikuwa
mbaya sana kwa sababu lile basi lilikuwa likibiringika kama chupa,
hivyo watu wanatupwa madirishani na kisha gari linawalalia ndio
mazingira watu walivyopoteza maisha.
OMG…!!!
