
KEPTENI wa Manchester United Wayne
Rooney hayumo kwenye Kikosi cha Timu hiyo kilichoruka kwenda Rotterdam kucheza
na Klabu ya Netherlands Feyenoord katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi A la UEFA
EUROPA LIGI.
Wengine ambao hawamo kwenye Kikosi
hicho cha Wachezaji 20 ni Luke Shaw, Antonio Valencia na Jesse Lingard.
Maneja Jose Mourinho amesema Rooney
amecheza Mechi zote za England na Man United na hivyo amepumzishwa ile awe
freshi kwa ajili ya tripu yao ya Ugenini hapo Jumapili wakicheza kwenye EPL,
Ligi Kuu England na Watford.
Kuhusu ushiriki wao kwenye
Mashindano haya, Morinho amekiri Klabu haikutaka kuwemo lakini maadamu wamo
basi watawania kutwaa Ubingwa.
Ameeleza: "Si ndoto ya kila
Mchezaji mkubwa lakini hatumo CHAMPIONZ LIGI. Lazima tuyatizame Mashindano haya
kwa heshima. Tunataka tufanye vyema!"
Mbali ya Marcus Rashford kuanza
Mechi hii kama Mourinho alivyodokeza, wengine wanaotarajiwa kucheza ni Marcos
Rojo atakaechukua nafasi ya Luke Shaw pamoja na Michael Carrick, Matteo
Darmian, Timothy Fosu-Mensah na Memphis Depay.
=============
JE WAJUA?
Man United imeshacheza na Feyenoord
mara 2, kwenye Kundi lao la UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu wa 1997/98, na Man United
kushinda Mechi zote mbili ikiwemo 3-1 huko Uwanjani De Kuip ambako Andy Cole
alipiga Hetitriki.
==============
Wakati huo huo, Feyenoord
wamelazimika kupunguza uwezo wa Uwanja De Kuip na kuwa na Watazamaji 30,000 tu
ili kukwepa Adhabu zaidi toka UEFA kwani kwa sasa wapo kwenye Angalizo baada ya
fujo za Mashabiki wao Msimu uliopita na kupunguzwa huko kutasaidia udhibiti wa
fujo za Mashabiki.
Manchester United - Kikosi cha
Wachezaji 20: De Gea, Romero, Johnstone, Darmian, Bailly, Blind, Fosu-Mensah,
Rojo, Smalling, Carrick, Fellaini, Herrera, Mata, Memphis, Pogba, Schneiderlin,
Young, Ibrahimovic, Martial, Rashford.
UEFA EUROPA LIGI
Mechi za Ufunguzi
Alhamisi Septemba 15
KUNDI A: Feyenoord v Manchester
United, Zorya Luhansk v Fenerbahçe
KUNDI B: Young Boys v Olympiacos,
APOEL v Astana
KUNDI C: Mainz v St-Étienne,
Anderlecht v Qäbälä
KUNDI D: AZ Alkmaar v Dundalk,
Maccabi Tel-Aviv v Zenit
KUNDI E: Viktoria Plzeň v Roma,
Astra Giurgiu v Austria Wien
KUNDI F: Rapid Wien v Genk, Sassuolo
v Athletic Club
KUNDI G: Standard Liège v Celta
Vigo, Panathinaikos v Ajax
KUNDI H: Konyaspor v Shakhtar
Donetsk, Braga v Gent
KUNDI I: Salzburg v Krasnodar, Nice
v Schalke
KUNDI J: Qarabağ v Slovan Liberec,
PAOK v Fiorentina
KUNDI K: Inter Milan v Hapoel
Beer-Sheva, Southampton v Sparta Praha
KUNDI L: Osmanlıspor v Steaua
Bucureşti, Villarreal v Zürich