POLISI - OLE WAO WATAKAOKUTWA NA SILAHA HARAMU - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Friday, 22 April 2016

POLISI - OLE WAO WATAKAOKUTWA NA SILAHA HARAMU

Uhalifu wa kutumia silaha uliokithiri nchini huenda ukapungua au kumalizika kabisa kuanzia Julai Polisi itakapofanya msako wa silaha haramu zinazokadiriwa kufikia kati ya 500 na 5,000 zilizomo mikononi mwa wahalifu.
Msako huo utafanyika baada ya kukamilika utaratibu wa kuhakiki silaha unaofanywa hivi sasa, watu wote wanaomiliki silaha wanatakiwa kuzipeleka makao makuu wa polisi wilaya kuonyesha nyaraka za umiliki au kuzisalimisha. Baada ya miezi mitatu iliyoanza Machi, watakaokutwa nazo watahesabiwa ni wahalifu na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Idadi ya silaha haramu zilizopo mikononi mwa wahalifu haijulikani, lakini Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athuman anasema kwa kuangalia rekodi ya silaha zilizokamatwa katika msako mwaka jana zinakaribia 500.
Kwa mujibu wa Athumani, mwaka uliopita (Januari hadi Desemba 2015), polisi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama maeneo mbalimbali nchini walikamata silaha 492 ambazo uchunguzi unaonyesha zinaingizwa kinyemela na makundi ya wahalifu.
“Silaha hizo kwa kiwango kikubwa, zinapitia mikoa yenye mipaka na nchi jirani ambako kuna mapigano ya wenyewe
kwa wenyewe, makundi ya uhalifu kama Al Shabaab na kwenye nchi ambazo kuna wapiganaji maeneo ya misituni,” anasema Athumani.