YANGA YARUDI KILELENI, YASHINDA MBILI BILA, KESHO SIMBA UIWANJANI - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Saturday, 6 May 2017

YANGA YARUDI KILELENI, YASHINDA MBILI BILA, KESHO SIMBA UIWANJANI

Yanga Africans wamefanikiwa kurudi kileleni katika msimamo wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara baada ya kuifunga bao 2-0 timu ya Tanzania Prisons katika mchezo ulimalizika jioni ya leo uwanja wa taifa Dar Es Salaam

Yanga sasa wametimiza pointi 59 sawa  na Simba lakini wakirejea kileleni kwa uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Yanga waliingia dimbani wakiwa na shauku ya kuzichukua pointi hizo tatu muhimu huku Prisons
wakionekana kucheza kwa tahadhari kila wakakati. 

Kipindi cha kwanza kilimalizika bila ya kufungana licha ya Yanga kutawala zaidi pambano.

Mabadiliko ya kipindi cha pili ya kumtoa beki Hassan Kessy na kumpa nafasi Juma Abdul na pia kumuingiza Haruna Niyonzima kuliiongezea kasi safu ya ushambuliaji ya Yanga.

Mshambuliaji Amissi Tambwe alifanikiwa kuunganisha kwa kichwa krosi ya Juma Abdul kutokea upande wa kushoto mnamo dakika ya 71.

Dakika nne baadaye Obrey Chirwa aliihakikishia Yanga ushindi kwa bao lake la kumi na la pili alipomalizia kazi nzuri ya Haruna Niyonzima.

Matokeo mengine:
Toto Africans 2-1 Jkt Ruvu
Ruvu Shouting 1-1 Kagera Suger
Majimaji 3-0 Mwadui Fc

Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mchezo mmoja ambapo Simba sc itacheza na African Lyon katika uwanja wa taifa Dar es salaam.