PRISONS YATAMBA KUIFUNGA YANGA ROBO FAINALI FA - CAPITAL TZ BLOG DODOMA

Latest

BANNER 728X90

Thursday, 20 April 2017

PRISONS YATAMBA KUIFUNGA YANGA ROBO FAINALI FA

KOCHA Mkuu wa Prisons ya Mbeya, Abdallah Mohammed ‘Bares’ amesema kwamba wataing’oa Yanga katika Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) keshokutwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

kocha huyo amesema kuwa anawaheshimu Yanga SC kama timu kubwa na mabingwa wa Tanzania, hivyo wanajua mchezo utakuwa mgumu, lakini watajitahidi kupigania ushindi.


Yanga watakuwa wenyeji wa Prisons Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa mwisho wa Robo Fainali ya Kombe la ASFC kutafuta tiketi ya kuungana na Simba, Azam FC na Mbao FC ambazo tayari zimetinga Nusu Fainali ya michuano hiyo.