Wakazi wa manispaa ya morogoro leo hii
wamejitokeza kuilaki timu ya Mkoa wa Morogoro iliyofanikiwa kubeba taji la
michuano ya Airtel Rising Stars siku ya jana ilipoichapa timu ya mkoa wa Ilala
bao 1-0.
Akizungumza wakati akikabidhiwa kikombe cha ushindi
na timu hiyo mkuu wa wilaya ya Morogoro Bi Regina Chonjo amewapongeza vijana
hao kwa ushindi walioupata huku akiwataka wazazi na walezi kutoa fursa kwa
watoto kushiriki kwenye michezo.
Naye mstahiki meya wa manispaa ya morogoro ambaye ni
mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa morogoro Pascal Kihanga amesema kuwa mkoa
wa morogoro umekuwa na historia nzuri katika michezo licha ya kutokuwa katika
ushirikiano kwenye siku za hivi karibuni na akatoa shukrani kwa taasisi sita zilizounda
wachezaji hao.


